28 Wanaume, wanabiashara Wamidiani,+ wakapitia hapo. Basi wakamvuta na kumpandisha Yosefu kutoka katika lile shimo la maji+ kisha wakamuuza kwa wale Waishmaeli kwa vipande 20 vya fedha.+ Mwishowe wanabiashara hao wakampeleka Yosefu Misri.
15 Baadaye Farao akasikia juu ya jambo hilo, naye akajaribu kumuua Musa;+ lakini Musa akakimbia+ toka kwa Farao apate kuishi katika nchi ya Midiani;+ naye akaketi kando ya kisima.
2 Nao mkono wa Midiani ukawa na nguvu juu ya Israeli.+ Kwa sababu ya Midiani, wana wa Israeli walijifanyia maghala ya chini ya udongo yaliyokuwa katika milima, na mapango na mahali palipo pagumu kufikiwa.+