Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 4:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Naye Yehova akamwambia Musa: “Ukisha kwenda na kurudi Misri hakikisha umefanya miujiza yote ambayo nimeitia mkononi mwako mbele ya Farao.+ Mimi nami, nitauacha moyo wake uwe mkaidi;+ naye hatawaruhusu watu waende zao.+

  • Kutoka 8:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Hata hivyo, Farao akaufanya moyo wake uwe mgumu wakati huu pia wala hakuwaruhusu watu waende zao.+

  • Kutoka 14:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Mimi nami, tazama, nitaiacha mioyo ya Wamisri iwe mikaidi,+ ili waingie kuwafuatilia wao nami nijipatie utukufu kupitia kwa Farao na majeshi yake yote, magari yake ya vita na askari wake wapanda-farasi.+

  • Yoshua 11:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Kwa kuwa hiyo ndiyo iliyokuwa njia ya Yehova ya kutenda, kuacha mioyo yao iwe migumu+ ili watangaze vita juu ya Israeli, kusudi awaangamize, ili wasipate kibali,+ bali ili yeye apate kuwaangamiza, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Naye akamwasi hata Mfalme Nebukadneza,+ aliyekuwa amemwapisha kwa Mungu;+ naye akaendelea kuifanya shingo yake kuwa ngumu+ na kuufanya moyo wake kuwa mgumu+ ili asirudi kwa Yehova Mungu wa Israeli.

  • Zaburi 75:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Msiinue pembe yenu juu.

      Msiseme mkiwa na shingo yenye kiburi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki