10Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Ingia ndani kwa Farao, kwa sababu mimi—mimi nimeuacha moyo wake na mioyo ya watumishi wake iwe migumu,+ ili niweke ishara zangu hizi mbele yake,+
10 Na Musa na Haruni wakafanya miujiza yote hiyo mbele ya Farao;+ lakini Yehova alikuwa akiuacha moyo wa Farao uwe mkaidi, hivi kwamba hakuwaruhusu wana wa Israeli waende zao kutoka katika nchi yake.+
30 Naye Sihoni mfalme wa Heshboni hakuturuhusu tupite katikati yake, kwa sababu Yehova Mungu wako alikuwa ameiacha roho yake iwe kaidi+ na moyo wake uwe mgumu, ili amtie mkononi mwako kama ilivyo leo hii.+
6 Pia, kwa nini mfanye mioyo yenu kuwa migumu kama vile Misri na Farao walivyofanya mioyo yao kuwa migumu?+ Je, haikuwa ni mara tu Yeye alipowatendea vikali+ ndipo walipowaachilia waende zao, nao wakaenda zao?+
20 Lakini moyo wake ulipojivuna na roho yake ikawa ngumu, akatenda kwa kimbelembele,+ alishushwa kutoka katika kiti cha ufalme wake, akaondolewa heshima yake.+