3 Ndipo Musa akamwambia Haruni: “Hivi ndivyo Yehova amesema, ‘Na nitakaswe+ kati ya wale walio karibu nami,+ nami nitukuzwe mbele ya uso wa watu wote.’”+ Naye Haruni akakaa kimya.
14 kwa sababu ninyi mliasi agizo langu katika nyika ya Zini kusanyiko lilipogombana,+ juu ya kunitakasa+ kando ya maji mbele ya macho yao. Hayo ndiyo maji ya Meriba+ huko Kadeshi+ katika nyika ya Zini.”+
51 Kwa sababu ninyi mlitenda isivyofaa kunielekea mimi+ katikati ya wana wa Israeli kwenye maji ya Meriba+ ya Kadeshi katika nyika ya Zini; kwa sababu ninyi hamkunitakasa mimi katikati ya wana wa Israeli.+
13 Yehova wa majeshi—yeye Ndiye mnayepaswa kuona kuwa mtakatifu,+ naye ndiye anayepaswa kuwa kitu cha kuogopwa nanyi,+ na Yeye ndiye anayepaswa kuwatetemesha ninyi.”+
11 “Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu+ na heshima+ na nguvu,+ kwa sababu uliumba vitu vyote,+ na kwa sababu ya mapenzi+ yako vilikuwako navyo vikaumbwa.”+