Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 21:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Basi kukawa na njaa+ katika siku za Daudi kwa miaka mitatu, mwaka baada ya mwaka; naye Daudi akatafuta shauri mbele za uso wa Yehova. Kisha Yehova akasema: “Kuna hatia ya damu juu ya Sauli na juu ya nyumba yake, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”+

  • Methali 6:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 macho ya majivuno,+ ulimi wa uwongo,+ na mikono inayomwaga damu isiyo na hatia,+

  • Methali 8:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia yaliyo mabaya.+ Nimechukia kujiinua na kiburi+ na njia mbaya na kinywa kipotovu.+

  • Zekaria 5:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 ‘Nimeifanya hiyo iende,’ asema Yehova wa majeshi, ‘nayo itaingia katika nyumba ya mwizi na katika nyumba ya mtu anayefanya kiapo rasmi katika jina langu kwa uwongo;+ nayo itakaa katikati ya nyumba yake na kuiangamiza pamoja na mbao zake na mawe yake.’ ”+

  • Zekaria 8:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Nanyi msipangiane mabaya mioyoni mwenu,+ wala msipende kiapo chochote cha uwongo;+ kwa maana nimeyachukia mambo hayo yote,’+ asema Yehova.”

  • Malaki 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Nami nitawakaribia ninyi ili kuhukumu,+ nami nitakuwa shahidi wa haraka+ juu ya walozi,+ na juu ya wazinzi,+ na juu ya wale wanaoapa kwa uwongo,+ na juu ya wale wanaoupunja mshahara wa mfanyakazi,+ na mjane+ na mvulana asiye na baba,+ na wale wanaomfukuza mkaaji mgeni,+ wala hawakuniogopa mimi,”+ Yehova wa majeshi amesema.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki