-
Waamuzi 10:6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Na wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ nao wakaanza kutumikia Mabaali+ na sanamu za Ashtorethi+ na miungu ya Siria+ na miungu ya Sidoni+ na miungu ya Moabu+ na miungu ya wana wa Amoni+ na miungu ya Wafilisti.+ Basi wakamwacha Yehova wala hawakumtumikia yeye.+
-
-
1 Samweli 7:3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Na Samweli akaiambia nyumba yote ya Israeli: “Ikiwa mnarudi kwa Yehova+ kwa mioyo yenu yote, ondoeni miungu ya kigeni iliyo katikati yenu+ na pia zile sanamu za Ashtorethi,+ nanyi mwelekeze mioyo yenu kwa Yehova bila kuyumba-yumba, mkamtumikie yeye peke yake,+ naye atawakomboa kutoka mkono wa Wafilisti.”+
-
-
2 Wafalme 23:13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Na mahali pa juu palipokuwa mbele+ ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa Mlima wa Uharibifu, ambapo Sulemani+ mfalme wa Israeli alijenga kwa ajili ya Ashtorethi+ chukizo la Wasidoni na kwa ajili ya Kemoshi+ chukizo la Moabu na kwa ajili ya Milkomu+ chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapafanya pasifae kwa ibada.
-