11 Na ikawa kwamba walipokuwa wanakimbia kutoka mbele ya Israeli, wakiwa kwenye mteremko wa Beth-horoni, Yehova akawatupia mawe+ makubwa kutoka mbinguni mpaka Azeka, nao wakafa. Wale waliokufa kutokana na hayo mawe ya mvua walikuwa wengi kuliko wale ambao wana wa Israeli waliwaua kwa upanga.
15 Ndipo Yehova akaanza kumvuruga+ Sisera na magari yake yote ya vita na kambi yote kwa makali ya upanga mbele ya Baraka. Mwishowe Sisera akashuka kutoka garini, akaanza kukimbia kwa miguu.
10 Na ikawa kwamba Samweli alipokuwa akitoa lile toleo la kuteketezwa, Wafilisti wakasonga karibu ili kupigana na Israeli. Na huko Yehova akafanya kuwe na mngurumo wa sauti kubwa+ siku hiyo juu ya Wafilisti, ili awavuruge;+ nao wakashindwa mbele ya Israeli.+