10 Basi roho+ ya Yehova ikaja juu yake, naye akawa mwamuzi wa Israeli. Alipoenda vitani, Yehova akamtia Kushan-rishathaimu mfalme wa Siria mkononi mwake na mkono wake ukamshinda nguvu+ Kushan-rishathaimu.
29 Sasa roho ya Yehova ikaja juu ya Yeftha,+ naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita katika Mispe la Gileadi,+ na kutoka Mispe la Gileadi akapita kwenda kwa wana wa Amoni.
6 Ndipo roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu yake,+ naye akampasua vipande viwili, kama vile mtu anavyompasua mwana-mbuzi vipande viwili, wala hapakuwa na kitu chochote mkononi mwake. Naye hakumwambia baba yake wala mama yake jambo alilokuwa amefanya.
14 Naye akaja mpaka Lehi, nao Wafilisti wakapaaza sauti kwa shangwe walipokutana naye.+ Na roho ya Yehova+ ikaanza kutenda kazi juu yake, na zile kamba zilizokuwa kwenye mikono yake zikawa kama nyuzi za kitani ambazo zimeunguzwa kwa moto,+ nazo pingu zake zikayeyuka kutoka kwenye mikono yake.
11 Na mtu akaanza kuzikumbuka siku za zamani za kale, Musa mtumishi wake: “Yuko wapi Yeye aliyewapandisha kutoka katika bahari+ pamoja na wachungaji wa kundi lake?+ Yuko wapi Yeye aliyetia ndani yake roho Yake takatifu?+
6 Basi akajibu na kuniambia: “Hili ndilo neno la Yehova kwa Zerubabeli, akisema, “Si kwa jeshi,+ wala kwa nguvu,+ bali kwa roho yangu,”+ Yehova wa majeshi amesema.