Zekaria
4 Na malaika aliyekuwa akisema nami akarudi na kuniamsha, kama mtu anayeamshwa kutoka katika usingizi.+ 2 Ndipo akaniambia: “Unaona nini?”+
Basi nikasema: “Nimeona, na tazama! kuna kinara cha taa, chote ni cha dhahabu,+ na bakuli liko juu yake. Na taa zake saba ziko juu yake, ndiyo, saba;+ na taa zilizo juu yake zina mirija saba. 3 Na kuna mizeituni miwili kando yake,+ mmoja upande wa kuume wa bakuli na mwingine upande wake wa kushoto.”
4 Ndipo nikamuuliza malaika aliyekuwa akisema nami: “Vitu hivi vinamaanisha nini, bwana wangu?”+ 5 Basi malaika aliyekuwa akisema nami akajibu na kuniambia: “Je, kweli wewe hujui maana ya vitu hivi?”
Ndipo nikasema: “Sijui, bwana wangu.”+
6 Basi akajibu na kuniambia: “Hili ndilo neno la Yehova kwa Zerubabeli, akisema, “Si kwa jeshi,+ wala kwa nguvu,+ bali kwa roho yangu,”+ Yehova wa majeshi amesema. 7 Wewe ni nani, Ee mlima mkubwa?+ Utakuwa nchi tambarare mbele ya Zerubabeli.+ Naye ataleta jiwe la juu kabisa.+ Nalo litapaaziwa sauti:+ “Linavutia kama nini! Linavutia kama nini!” ’ ”+
8 Kisha neno la Yehova likaendelea kunijia, likisema: 9 “Mikono ya Zerubabeli ndiyo imeweka msingi wa nyumba hii,+ na mikono yake mwenyewe itaikamilisha.+ Nanyi mtajua ya kuwa Yehova wa majeshi amenituma kwenu ninyi.+ 10 Kwa maana ni nani ameidharau siku ya mambo madogo?+ Nao watafurahi+ na kuona timazi mkononi mwa Zerubabeli. Haya saba ndiyo macho ya Yehova.+ Yanaenda huku na huku duniani kote.”+
11 Nami nikamjibu, nikamwambia: “Hii mizeituni miwili upande wa kuume wa kinara cha taa na upande wake wa kushoto inamaanisha nini?”+ 12 Kisha nikamjibu, nikamwambia mara ya pili: “Yale mafungu mawili ya matawi ya mizeituni ambayo, kwa njia ya mifereji miwili ya dhahabu, yanamimina umajimaji wa dhahabu kutoka ndani yake ni nini?”
13 Basi akaniambia: “Je, kweli wewe hujui maana ya vitu hivi?”
Ndipo nikasema: “Sijui, bwana wangu.”+
14 Ndipo akasema: “Hawa ndio wale watiwa-mafuta+ wawili wanaosimama kando ya Bwana wa dunia yote.”+