10 Basi wakatoka hapo wakaenda kwenye kilima, na tazama, kulikuwa na kikundi cha manabii kikija kumpokea; ndipo mara moja roho ya Mungu ikaanza kutenda kazi juu yake,+ naye akaanza kusema kama nabii+ katikati yao.
23 Naye akaendelea na safari yake kutoka hapo mpaka Naiothi katika Rama, na roho+ ya Mungu ikaja juu yake, ndiyo, juu yake, naye akaendelea kutembea na kutenda kama nabii mpaka alipoingia Naiothi katika Rama.
29 Na ikawa kwamba mara tu mchana ulipokwisha nao wakazidi kutenda kama manabii+ mpaka wakati wa kutolewa kwa toleo la nafaka, hapakuwa na sauti yoyote, wala hapakuwa na yeyote aliyejibu, wala aliyewasikiliza.+
10 Sasa mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi kila mmoja juu ya kiti chake cha ufalme, wakiwa wamevaa mavazi ya kifalme,+ katika uwanja wa kupuria kwenye mwingilio wa lango la Samaria; na manabii wote walikuwa wakitenda kama manabii mbele yao.+