30 Sasa Yosefu alikuwa akiharakisha, kwa sababu hisia zake za ndani zilianza kusisimuka kumwelekea ndugu yake,+ hata akatafuta mahali pa kulilia, naye akaingia katika chumba cha ndani, akaanza kulia machozi humo.+
15 Je, mke anaweza kumsahau mtoto wake anayenyonya hivi kwamba asimhurumie mwana wa tumbo lake?+ Hata hawa wanawake wanaweza kusahau,+ lakini mimi mwenyewe sitakusahau wewe.+
20 “Je, Efraimu ni mwana mwenye thamani kwangu, au mtoto anayetendewa kwa upendo?+ Kwa maana kwa kiasi ninachosema vibaya juu yake bila shaka nitamkumbuka zaidi.+ Ndiyo sababu matumbo yangu yamekuwa na msukosuko kwa ajili yake.+ Kwa kuwa nitamhurumia kabisa,”+ asema Yehova.
8 “Nawezaje kukuacha, Ee Efraimu?+ Nawezaje kukutoa, Ee Israeli?+ Nawezaje kukufanya uwe kama Adma?+ Nawezaje kukuweka uwe kama Seboiimu?+ Moyo wangu umebadilika ndani yangu;+ na wakati huohuo huruma zangu zimewaka.