9 Kwa maana, kwa habari ya Yehova, macho+ yake yanaenda huku na huku duniani+ kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo+ wao ni mkamilifu kumwelekea yeye. Umetenda kwa upumbavu+ kwa habari hii, kwa maana tangu sasa na kuendelea kutakuwa na vita juu yako.”+
6 huyo Ezra alitoka Babiloni; naye alikuwa mwandikaji stadi+ katika sheria ya Musa,+ ambayo Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa, hata mfalme akampa maombi yake yote, kulingana na mkono wa Yehova Mungu wake juu yake.+
28 Naye amenipa fadhili zenye upendo+ mbele ya mfalme na washauri+ wake na kuhusu wakuu wote wa mfalme wenye nguvu. Mimi nami nikajitia nguvu kulingana na mkono+ wa Yehova Mungu wangu juu yangu, nami nikawakusanya wakuu kutoka katika Israeli ili waende pamoja nami.
6 Basi akajibu na kuniambia: “Hili ndilo neno la Yehova kwa Zerubabeli, akisema, “Si kwa jeshi,+ wala kwa nguvu,+ bali kwa roho yangu,”+ Yehova wa majeshi amesema.