29 Mungu akaendelea kusema: “Tazama nimewapa mimea yote inayozaa mbegu iliyo juu ya uso wa dunia yote na kila mti ambao una matunda ya mti unaozaa mbegu.+ Na iwe chakula kwenu.+
25 “Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi: Acheni kuhangaika+ juu ya nafsi zenu kuhusu kile mtakachokula au kile mtakachokunywa, au juu ya miili yenu kuhusu kile mtakachovaa.+ Je, nafsi haimaanishi zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?+
30 Basi, ikiwa Mungu huivika hivyo mimea ya shambani, ambayo ipo hapa leo na kesho hutupwa ndani ya jiko, je, yeye hataona ni afadhali zaidi awavike, ninyi wenye imani kidogo?+
28 Ikiwa, basi, Mungu huvika hivyo mimea iliyo shambani ambayo leo ipo na kesho hutupwa ndani ya jiko, basi atawavika ninyi hata zaidi, ninyi wenye imani kidogo!+
16 “Kwa maana Mungu aliupenda+ ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee,+ ili kila mtu anayemwamini+ asiangamizwe+ bali awe na uzima wa milele.+
17 ijapokuwa, kwa kweli, hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema,+ akiwapa ninyi mvua+ kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamfu.”+