20 Kwa upande wenu, ninyi mlikuwa na uovu akilini mwenu kunielekea mimi. Mungu alikuwa na wema akilini kwa kusudi la kutenda kama ilivyo leo hii ili kuhifadhi hai watu wengi.+
24 Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mbegu ya ngano isipoanguka katika udongo na kufa, hiyo hubaki ikiwa mbegu moja tu; lakini ikifa,+ ndipo hiyo huzaa matunda mengi.
11 Tazama! Tunawatangaza kuwa wenye furaha wale ambao wamevumilia.+ Mmesikia juu ya uvumilivu wa Ayubu+ nanyi mmeona matokeo ambayo Yehova alileta,+ kwamba Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.+