3 ndipo Yehova Mungu wako atakaporudisha mateka+ wako pia na kukuonyesha rehema+ na kukukusanya tena kutoka kwa vikundi vyote vya watu ambako Yehova Mungu wako amekutawanya.+
9 Mtakaporudi kwangu+ na kuzishika amri zangu+ na kuzifanya,+ hata watu wenu waliotawanywa wawe katika mwisho wa mbingu, kutoka huko nitawakusanya+ na kuwaleta+ mahali ambapo nimepachagua ili jina langu likae hapo.’+
14 “Rudini, enyi wana waasi,’+ asema Yehova. “Kwa maana mimi nimekuwa mume wenu;+ nami nitawachukua, mmoja kutoka katika jiji moja na wawili kutoka katika familia moja, nami nitawaleta ninyi Sayuni.+
14 Nami nitakusanya na kurudisha mateka wa watu wangu Israeli,+ nao watajenga majiji yaliyofanywa ukiwa na kukaa ndani yake,+ watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake, watafanyiza bustani na kula matunda yake.’+