9 (Nyakati za kale katika Israeli, mtu alikuwa akisema hivi akienda kumtafuta Mungu: “Haya njooni, na twende kwa mwonaji.”+ Kwa maana nabii wa leo alikuwa akiitwa mwonaji nyakati za kale.)
14 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Manabii wanatoa unabii wa uwongo katika jina langu.+ Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru wala kusema nao.+ Maono ya uwongo na uaguzi na kitu kisicho na thamani+ na udanganyifu wa moyo wao ndiyo mambo wanayowaambia ninyi kwa njia ya unabii.+
15 “‘Kwa maana mimi sikuwatuma,’ asema Yehova, ‘lakini wanatoa unabii katika jina langu kwa uwongo, kusudi niwatawanye,+ nanyi mwangamie,+ ninyi pamoja na wale manabii wanaowatolea unabii.’”+