23 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja, yenye thamani ya vipande elfu moja vya fedha,+ patakuwa—kwa ajili ya vichaka vya miiba na kwa ajili ya magugu.+
13 “‘Nitakapokuwa nikikusanya, nitawamaliza,’ asema Yehova.+ ‘Hakutakuwa na zabibu juu ya mzabibu,+ wala hakutakuwa na tini juu ya mtini, na hakika majani yatakauka. Na vitu ninavyowapa vitapita kando yao.’”
12 Nami nitaufanya kuwa ukiwa mzabibu+ wake na mtini+ wake, ambao amesema hivi kuuhusu: “Hizo ni zawadi zangu nilizopewa, ambazo wale wanaonipenda kwa tamaa nyingi wamenipa”; nami nitazifanya kuwa msitu,+ na mnyama wa mwituni atazila.
13 Na mali yao itakuwa ya kunyakuliwa na nyumba zao zitakuwa mahame yenye ukiwa.+ Nao watajenga nyumba, lakini hawatakaa humo;+ nao watapanda mashamba ya mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+