Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezra 1:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 1 Na katika mwaka wa kwanza wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi, ili neno la Yehova kwa kinywa cha Yeremia+ litimizwe, Yehova aliiamsha+ roho ya Koreshi mfalme wa Uajemi, hivi kwamba akatangaza mwito+ katika utawala wake wote, na pia kwa maandishi,+ akisema:

  • Isaya 41:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Nimemwamsha mtu kutoka kaskazini, naye atakuja.+ Kutoka mashariki+ ataliitia jina langu. Naye atakuja juu ya watawala-wasaidizi kana kwamba wao ni udongo+ na kama vile mfinyanzi anayekanyagia chini chombo kibichi.

  • Isaya 45:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 45 Yehova amemwambia hivi mtiwa-mafuta wake,+ Koreshi, ambaye mkono wake wa kuume nimeushika,+ ili kuyatiisha mataifa mbele yake,+ hivi kwamba nivifungue viuno vya wafalme; nifungue mbele yake milango yenye pande mbili, hivi kwamba hata malango hayatafungwa:

  • Isaya 46:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yeye anayemwita ndege mwenye kuwinda kutoka mashariki,+ kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza shauri langu.+ Mimi nimesema hilo; pia nitalitimiza.+ Nimelifanyiza, pia nitalitenda.+

  • Danieli 10:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi kuna jambo alilofunuliwa Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza;+ na jambo hilo lilikuwa kweli, na kulikuwa na utumishi mkubwa wa kijeshi.+ Naye akaelewa jambo lile, naye akaelewa jambo lililoonwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki