Isaya
46 Beli+ ameinama,+ Nebo amejikunja; sanamu+ zao zimekuwa za wanyama-mwitu na za wanyama wa kufugwa, mizigo yao, vifurushi, mzigo wa kulemea wanyama waliochoka. 2 Watajikunja; wote watainama pamoja; hawawezi kwa vyovyote kuuponyosha+ mzigo, bali nafsi yao wenyewe itaenda utekwani.+
3 “Nisikilize mimi, Ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote mnaobaki wa nyumba ya Israeli,+ ninyi niliowachukua tangu tumboni, ambao mmechukuliwa toka tumbo la uzazi.+ 4 Hata uzeeni mwa mtu mimi ni Yeye yuleyule;+ na hata wakati wa kichwa chenye mvi cha mtu nitaendelea kubeba.+ Mimi mwenyewe hakika nitatenda,+ ili mimi mwenyewe nichukue na ili mimi mwenyewe nibebe na kuponyosha.+
5 “Ninyi mtanifananisha na nani+ au kunifanya kuwa sawa na nani au kunilinganisha na nani ili tuwe sawasawa?+ 6 Kuna wale wanaotoa dhahabu kwa wingi katika kikoba, nao hupima fedha kwa mizani. Wanamwajiri fundi wa chuma, naye huifanya kuwa mungu.+ Wanasujudu, ndiyo, wanainama.+ 7 Wao huichukua begani,+ huibeba na kuiweka mahali pake ili isimame tuli. Hiyo haisongi kutoka mahali pake inaposimama.+ Mtu hata huililia, lakini haijibu; haimwokoi mtu kutoka katika taabu yake.+
8 “Kumbukeni hili, ili mjipe moyo. Liwekeni moyoni,+ ninyi wakosaji.+ 9 Kumbukeni mambo ya kwanza ya zamani za kale,+ kwamba mimi ni Mungu+ wala hakuna Mungu mwingine,+ wala yeyote kama mimi;+ 10 Yeye anayetangaza tangu mwanzo ule mwisho,+ na kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa;+ Yeye anayesema, ‘Shauri langu mwenyewe litasimama,+ na kila jambo ambalo ni mapenzi yangu nitafanya’;+ 11 Yeye anayemwita ndege mwenye kuwinda kutoka mashariki,+ kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza shauri langu.+ Mimi nimesema hilo; pia nitalitimiza.+ Nimelifanyiza, pia nitalitenda.+
12 “Nisikilizeni, ninyi wenye moyo mkaidi,+ ninyi mlio mbali na uadilifu.+ 13 Nimeuleta karibu uadilifu wangu.+ Hauko mbali,+ na wokovu wangu hautachelewa.+ Nami nitaleta wokovu katika Sayuni, na kwa Israeli uzuri wangu.”+