20 “‘Kwa maana zamani nilivunja nira yako vipande-vipande;+ nilizikata pingu zako. Lakini ulisema: “Mimi sitatumikia,” kwa maana ulikuwa umelala huku umejinyoosha+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi,+ ukifanya ukahaba.+
16 Nawe ukachukua sehemu ya mavazi yako na kujifanyia mwenyewe mahali pa juu+ penye rangi mbalimbali nawe ukawa ukifanya ukahaba juu yake+—mambo hayo hayaingii, na hayapasi kutukia hivyo.
17 Nao wana wa Babiloni wakaendelea kumjia, kwenye kitanda cha wonyesho wa upendo, na kumtia unajisi kwa uasherati wao;+ nao wakaendelea kumtia unajisi, nayo nafsi yake ikaanza kugeukia mbali nao kwa kuchukizwa.