4 Naye hakika atafanya hukumu kati ya mataifa+ na kunyoosha mambo+ kuhusu vikundi vingi vya watu.+ Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.+ Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.+
9 Hawatasababisha madhara+ yoyote wala kusababisha uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu;+ kwa maana dunia hakika itajawa na kumjua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.+
14 Utafanywa imara katika uadilifu.+ Utakuwa mbali sana na ukandamizaji+—kwa maana hutaogopa yeyote—na jambo lolote lenye kutia hofu, kwa maana halitakuja karibu nawe.+
8 Nami nitapiga kambi kama mlinzi wa mbele kwa ajili ya nyumba yangu,+ ili kusiwe na mtu yeyote anayepita kati wala anayerudi; wala msimamizi wa kazi+ hatapita tena kwao, kwa maana sasa nimeyaona kwa macho yangu.+