16 Manase pia alimwaga kwa wingi sana damu isiyo na hatia,+ mpaka alipolijaza Yerusalemu kutoka mwisho huu mpaka mwisho ule, mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda dhambi kwa kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
4 na pia kwa sababu ya damu isiyo na hatia+ aliyokuwa amemwaga, hivi kwamba akalijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia, na Yehova hakukubali kutoa msamaha.+
2 ili kuwasukuma mbali watu wa hali ya chini kutoka kwenye kesi na kuwanyang’anya haki wale wanaoteseka kati ya watu wangu,+ ili wajane wawe nyara yao, na ili hata wapore wavulana wasio na baba!+
7 Miguu yao huendelea kukimbia kuelekea ubaya mtupu,+ nao wanafanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia.+ Mawazo yao ni mawazo yenye madhara;+ uporaji na mvunjiko zimo katika njia kuu zao.+
4 kwa sababu wameniacha+ mimi nao wamepafanya mahali hapa pasitambuliwe+ na kufukiza moshi wa dhabihu ndani yake kwa miungu mingine ambayo hawakuijua,+ wao pamoja na mababu zao na wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia.+
35 ili ije juu yenu damu yote ya uadilifu iliyomwagwa juu ya dunia,+ tangu damu+ ya Abeli+ mwadilifu mpaka damu ya Zekaria mwana wa Barakia, ambaye mlimuua katikati ya patakatifu na madhabahu.+