8 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu.+ Na jina la mama yake lilikuwa Nehushta binti ya Elnathani wa Yerusalemu.
9 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu+ na siku kumi katika Yerusalemu; naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
24 “‘Kama ninavyoishi,’ asema Yehova, ‘hata kama Konia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, angekuwa pete ya muhuri+ kwenye mkono wangu wa kuume, ningekung’oa wewe kutoka hapo!+
20 ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babiloni hakuchukua alipompeleka uhamishoni Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni, pamoja na watu wote wenye vyeo wa Yuda na Yerusalemu;+
4 “‘Na Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, pamoja na wahamishwa wote wa Yuda ambao wameenda Babiloni+ nitawarudisha tena mahali hapa,’ asema Yehova, ‘kwa maana nitaivunja nira+ ya mfalme wa Babiloni.’”