5 Ndipo vichwa+ vya upande wa baba vya Yuda na vya Benyamini na makuhani na Walawi wakasimama, ndiyo, kila mmoja ambaye Mungu wa kweli aliiamsha roho+ yake, ili kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova,+ iliyokuwa Yerusalemu.
3 Na vikundi vingi vya watu hakika vitaenda na kusema: “Njooni,+ twendeni juu kwenye mlima wa Yehova, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutatembea katika mapito yake.”+ Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.+
5 Wataendelea kuuliza njia ya kwenda Sayuni, nyuso zao zikiwa zimeelekezwa upande huo,+ wakisema, ‘Njooni, tujiunge pamoja na Yehova katika agano ambalo halitasahauliwa, linalodumu mpaka wakati usio na kipimo.’+
2 Na mataifa mengi hakika yatakwenda na kusema: “Njooni,+ twendeni juu kwenye mlima wa Yehova na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo;+ naye atatufundisha njia zake,+ nasi tutatembea katika mapito yake.”+ Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.+