Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 24:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 “Hupaswi kupotosha hukumu ya mkaaji mgeni+ au ya mvulana asiye na baba,+ nawe hupaswi kutwaa vazi la mjane kama rehani.+

  • Zaburi 82:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Iweni waamuzi kwa ajili ya mtu wa hali ya chini na mvulana asiye na baba.+

      Kwa mtu mwenye kuteseka na maskini, mtendeeni haki.+

  • Zekaria 7:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 wala msimpunje mjane+ yeyote na mvulana yeyote asiye na baba,+ wala mkaaji mgeni+ au mwenye kuteseka,+ wala msipangiane jambo lolote baya mioyoni mwenu.’+

  • Malaki 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Nami nitawakaribia ninyi ili kuhukumu,+ nami nitakuwa shahidi wa haraka+ juu ya walozi,+ na juu ya wazinzi,+ na juu ya wale wanaoapa kwa uwongo,+ na juu ya wale wanaoupunja mshahara wa mfanyakazi,+ na mjane+ na mvulana asiye na baba,+ na wale wanaomfukuza mkaaji mgeni,+ wala hawakuniogopa mimi,”+ Yehova wa majeshi amesema.

  • Yakobo 1:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Namna ya ibada iliyo safi+ na isiyotiwa unajisi+ kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuwatunza mayatima+ na wajane+ katika dhiki+ yao, na kuendelea kujitunza bila doa+ kutokana na ulimwengu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki