-
Ezekieli 3:20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Na mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu+ wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki nami nilazimike kuweka kikwazo mbele yake,+ yeye mwenyewe atakufa kwa sababu hukumwonya. Kwa sababu ya dhambi yake atakufa,+ na matendo yake ya uadilifu aliyoyatenda hayatakumbukwa,+ lakini damu yake nitaidai kutoka katika mkono wako mwenyewe.+
-
-
Ezekieli 18:24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 “ ‘Sasa, mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki;+ kulingana na machukizo yote ambayo mwovu ametenda yeye anaendelea kutenda+ naye anaishi, hakuna lolote la matendo yake ya uadilifu ambayo ametenda litakalokumbukwa.+ Atakufa kwa sababu ya ukosefu wake wa uaminifu ambao ametenda na kwa sababu ya dhambi ambayo ametenda.+
-