2 mimi pia nitayakusanya pamoja mataifa yote+ na kuwaleta kwenye bonde la Yehoshafati;+ nami huko nitajiweka katika hukumu nao kwa sababu ya watu wangu na urithi wangu Israeli,+ ambao wamewatawanya katikati ya mataifa; nao waligawanya nchi yangu mwenyewe.+
2 Nami nitakusanya mataifa yote yalete vita+ juu ya Yerusalemu; na jiji hilo litatekwa+ na nyumba zitanyakuliwa, na wanawake watalalwa kinguvu.+ Na nusu ya jiji itaenda uhamishoni;+ lakini watu watakaobaki,+ hawatakatiliwa mbali kutoka katika jiji hilo.+
14 Hayo, kwa kweli, ni maneno yanayoongozwa+ na roho waovu nayo yanafanya ishara,+ nayo yanakwenda kwa wafalme+ wa dunia nzima inayokaliwa,+ ili kuwakusanya pamoja kwa vita+ vya ile siku kuu+ ya Mungu Mweza-Yote.+
19 Nami nikamwona yule mnyama-mwitu+ na wafalme+ wa dunia na majeshi yao wamekusanyika pamoja ili kupigana vita+ na yule anayeketi juu ya farasi+ na jeshi lake.