4 Naye hakika atafanya hukumu kati ya mataifa+ na kunyoosha mambo+ kuhusu vikundi vingi vya watu.+ Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.+ Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.+
17 Badala ya shaba nitaingiza dhahabu,+ na badala ya chuma nitaingiza fedha, na badala ya miti, shaba, na badala ya mawe, chuma; nami nitaweka amani kuwa waangalizi+ wako na uadilifu kuwa wagawa-kazi wako.+
12 ‘Kwa maana kutakuwa na mbegu ya amani;+ mzabibu utazaa matunda yake,+ na dunia itatoa mazao yake,+ na mbingu zitatoa umande wake;+ nami nitawafanya mabaki+ ya watu hawa warithi vitu hivyo vyote.+