18 Nitawainulia wao nabii kutoka katikati ya ndugu zao, kama wewe;+ nami nitaweka maneno yangu katika kinywa chake,+ naye atasema nao yote nitakayomwamuru.+
6 Kwa maana kuna mtoto ambaye amezaliwa kwetu,+ kuna mwana ambaye tumepewa;+ na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake.+ Naye ataitwa jina Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele,+ Mkuu wa Amani.+
19 Naye akawaambia: “Mambo gani?” Wakamwambia: “Yale mambo kuhusu Yesu Mnazareti,+ aliyekuwa nabii+ mwenye nguvu katika kazi na neno mbele za Mungu na watu wote;
22 Kwa kweli, Musa alisema, ‘Yehova Mungu atawainulia kutoka kati ya ndugu zenu nabii kama mimi.+ Msikilizeni huyo kulingana na mambo yote anayowaambia ninyi.+