Methali 19:17 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 17 Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova,+ na Yeye atamlipa matendo yake.+ Methali 22:9 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, kwa maana amempa mtu wa hali ya chini chakula chake.+ Mhubiri 11:1 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 11 Tupa mkate+ wako juu ya uso wa maji,+ kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.+ Luka 6:38 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 38 Muwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi.+ Watawamwagia katika mfuko wa nguo zenu kipimo kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa pamoja na kufurika. Kwa maana kwa kipimo mnachopimia, watawapimia ninyi pia.”+
38 Muwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi.+ Watawamwagia katika mfuko wa nguo zenu kipimo kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa pamoja na kufurika. Kwa maana kwa kipimo mnachopimia, watawapimia ninyi pia.”+