Mhubiri
11 Tupa mkate+ wako juu ya uso wa maji,+ kwa maana baada ya siku nyingi utaupata tena.+ 2 Wape fungu watu saba, au hata wanane,+ kwa maana hujui ni msiba gani utakaotokea duniani.+
3 Mawingu yakijaa maji, humwaga mvua kubwa juu ya dunia;+ nao mti ukianguka kuelekea kusini au kaskazini, mahali hapo hapo ulipoanguka+ ndipo utakapokuwa.
4 Anayeuangalia upepo hatapanda mbegu; naye anayetazama mawingu hatavuna.+
5 Kama vile usivyoijua njia ya roho katika mifupa ndani ya tumbo lake mwenye mimba,+ vivyo hivyo hujui kazi ya Mungu wa kweli, anayefanya mambo yote.+
6 Asubuhi panda mbegu zako na mpaka jioni usiache mkono wako upumzike;+ kwa maana hujui ni wapi hii itafanikiwa,+ hapa au pale, au ikiwa zote mbili zitakuwa njema.
7 Nuru ni tamu pia, na ni vema macho yaone jua;+ 8 kwa maana mwanadamu akiishi miaka mingi, na aishangilie hiyo yote.+ Na azikumbuke siku za giza,+ ingawa huenda zikawa nyingi; kila siku ambayo imekuja ni ubatili.+
9 Ewe kijana, shangilia+ katika ujana wako, na moyo wako ukufanyie mema siku za ujana wako, nawe utembee katika njia za moyo wako na katika mambo ambayo macho yako yameona.+ Lakini ujue kwamba kwa ajili ya mambo yote hayo, Mungu wa kweli atakuleta hukumuni.+ 10 Kwa hiyo, ondoa masumbuko moyoni mwako, nawe uondolee mbali msiba kutoka katika mwili wako;+ kwa maana ujana na upeo wa maisha ni ubatili.+