32 Ndipo malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini umempiga punda wako mara hizi tatu? Tazama! Mimi—mimi nimekuja kukuzuia, kwa sababu njia yako imekwenda moja kwa moja kinyume cha mapenzi yangu.+
5 Na Yehova Mungu wako hakutaka kumsikiliza Balaamu;+ lakini Yehova Mungu wako kwa ajili yako aligeuza ile laana ikawa baraka,+ kwa sababu Yehova Mungu wako alikupenda.+
14 “ ‘Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako, kwamba unao hapo wale wanaolishika sana fundisho la Balaamu,+ aliyemfundisha Balaki+ kuweka kikwazo mbele ya wana wa Israeli, ili wale vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na kufanya uasherati.+