29 kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu+ na damu+ na vitu vilivyonyongwa+ na uasherati.+ Mkijiepusha kwa uangalifu na mambo haya,+ mtafanikiwa. Afya njema kwenu!”
11 Lakini sasa ninawaandikia ninyi mwache kuchangamana katika ushirika+ pamoja na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa+ au mwabudu-sanamu au mtukanaji au mlevi+ au mnyang’anyi, hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo.
5 Kwa maana mnajua hili, nanyi mnalitambua wenyewe, kwamba hakuna mwasherati+ au mtu asiye safi au mtu mwenye pupa+—maana yake ni kuwa mwabudu-sanamu—aliye na urithi wowote katika ufalme wa Kristo na wa Mungu.+