Zaburi 113 Msifuni Yah!+Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+Lisifuni jina la Yehova.+ 2 Jina la Yehova na libarikiwe+Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+ 3 Kutoka mapambazuko ya jua mpaka kutua kwake+Jina la Yehova ni la kusifiwa.+ 4 Yehova amekuwa juu ya mataifa yote;+Utukufu wake uko juu ya mbingu.+ 5 Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+Yeye anayefanya makao yake juu?+ 6 Yeye anajishusha kutazama mbingu na dunia,+ 7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi;+Humwinua maskini kutoka kwenye shimo la majivu,+ 8 Ili kumketisha pamoja na wenye vyeo,+Wenye vyeo kati ya watu wake.+ 9 Anampa mwanamke tasa makao katika nyumba+Kama mama ya wana aliye na shangwe.+Msifuni Yah!+