Waebrania
8 Basi kuhusu mambo yanayozungumzwa jambo kuu ni hili: Sisi tuna kuhani mkuu+ wa namna hii, naye ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Ukuu mbinguni,+ 2 mtumishi wa watu wote wa mahali patakatifu+ na wa hema la kweli, ambalo Yehova+ alisimamisha, na si mwanadamu.+ 3 Kwa maana kila kuhani mkuu huwekwa rasmi ili kutoa zawadi na dhabihu;+ kwa hiyo ilikuwa lazima pia kwa huyu kuwa na kitu fulani cha kutoa.+ 4 Sasa, kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani,+ kukiwa na watu ambao hutoa zawadi kulingana na Sheria, 5 lakini watu ambao wanatoa utumishi mtakatifu katika mfano wa uhalisi+ na kivuli+ cha vitu vya mbinguni; kama vile Musa, alipokuwa karibu kumaliza hema,+ alipewa amri ya kimungu:+ Kwa maana yeye anasema: “Uhakikishe kwamba umevifanya vitu vyote kulingana na mfano wake ambao wewe ulionyeshwa mlimani.”+ 6 Lakini sasa Yesu amepata utumishi wa watu wote ulio bora zaidi, hivi kwamba yeye pia ni mpatanishi+ wa agano lililo bora kwa kulinganishwa,+ ambalo limefanywa imara kisheria juu ya ahadi zilizo bora.+
7 Kwa maana ikiwa agano lile la kwanza lingekuwa bila kosa, mahali hapangetafutwa kwa ajili ya la pili;+ 8 kwa maana yeye anawalaumu wale watu anaposema: “ ‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitafanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda;+ 9 si kulingana na lile agano+ ambalo nilifanya pamoja na mababu zao katika ile siku nilipowashika mkono na kuwatoa katika nchi ya Misri,+ kwa sababu hawakuendelea kulishika agano langu,+ hivi kwamba nikaacha kuwajali,’ asema Yehova.”+
10 “ ‘Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova. ‘Nitazitia sheria zangu katika akili yao, nami nitaziandika katika mioyo yao.+ Nami nitakuwa Mungu wao,+ nao watakuwa watu wangu.+
11 “ ‘Nao hawatafundishana kwa vyovyote kila mtu na raia mwenzake wala kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”+ Kwa maana wote watanijua mimi,+ kuanzia yule aliye mdogo zaidi mpaka yule aliye mkubwa zaidi kati yao. 12 Kwa maana nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya uadilifu, nami sitazikumbuka+ tena dhambi+ zao hata kidogo.’ ”
13 Kwa kusema “agano jipya,” Yeye amelifanya lile la zamani kuchakaa.+ Basi kile kinachofanywa kuchakaa na kuzeeka kiko karibu kutoweka.+