Zaburi
Muziki, wimbo, kwa ajili ya siku ya sabato.
92 Ni vema kumtolea Yehova shukrani+
Na kulipigia jina lako muziki, ewe Uliye Juu Zaidi;+
2 Kutangaza asubuhi fadhili zako zenye upendo+
Na nyakati za usiku uaminifu wako.+
3 Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,+
Kwa muziki unaovuma wa kinubi.+
4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya utendaji wako;
Kwa sababu ya kazi za mikono yako, ninapiga vigelegele kwa shangwe.+
7 Wakati waovu wanapochipuka kama majani+
Na wote wanaotenda mambo yenye kuumiza wanapochanuka,
Ni ili wao wapate kuangamizwa milele.+
8 Lakini wewe uko juu mpaka wakati usio na kipimo, Ee Yehova.+
9 Kwa maana, tazama! adui zako, Ee Yehova,+
Kwa maana, tazama! adui zako mwenyewe wataangamia;+
Wote wanaofanya mambo yenye kuumiza watatenganishwa.+