Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 40:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi,+

      Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea;+

      Hakuna wa kulinganishwa nawe.+

      Ikiwa ningetaka kueleza na kusema juu yake,

      Zimekuwa nyingi sana kuliko vile ninavyoweza kusimulia.+

  • Zaburi 66:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Mwambieni Mungu: “Jinsi kazi zako zilivyo zenye kuogopesha!+

      Kwa sababu ya wingi wa nguvu zako, adui zako watakujia wakitetemeka.+

  • Zaburi 104:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova!+

      Zote umezifanya kwa hekima.+

      Dunia imejaa vitu ulivyotokeza.+

  • Zaburi 145:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Kizazi baada ya kizazi kitazipongeza kazi zako,+

      Nao watatangaza juu ya matendo yako ya nguvu.+

  • Zaburi 150:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Msifuni kwa kazi zake zenye nguvu.+

      Msifuni kulingana na wingi wa ukuu wake.+

  • Mhubiri 3:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Amefanya kila kitu kiwe chenye kupendeza kwa wakati wake.+ Tena wakati usio na kipimo ameuweka ndani ya moyo wao,+ ili mwanadamu asiweze kugundua kazi ambazo Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mpaka mwisho.+

  • Ufunuo 15:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Nao wanaimba wimbo wa Musa+ mtumwa wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo,+ wakisema:

      “Matendo yako ni makuu na ya ajabu,+ Yehova Mungu, Mweza-Yote.+ Njia zako ni za uadilifu na za kweli,+ Mfalme wa umilele.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki