1 Mambo ya Nyakati
13 Na Daudi akashauriana na wakuu wa maelfu na wa mamia na kila kiongozi;+ 2 na Daudi akaliambia kutaniko lote la Israeli: “Ikiwa vema kwenu na kukubalika kwa Yehova, Mungu wetu, na tutume watu kwa ndugu zetu waliobaki katika nchi zote za Israeli+ na pamoja nao makuhani+ na Walawi+ katika majiji+ yao yenye viwanja vya malisho, ili wajikusanye pamoja kwetu. 3 Nasi tulete sanduku+ la Mungu wetu kwetu.” Kwa maana hawakuwa wamelitunza katika siku za Sauli.+ 4 Basi kutaniko lote wakasema ifanywe hivyo, kwa maana jambo hilo lilionekana kuwa jema machoni pa watu wote.+ 5 Basi Daudi akakusanya+ Israeli wote kuanzia mto wa Misri+ mpaka maingilio ya Hamathi,+ ili kulileta sanduku+ la Mungu wa kweli kutoka Kiriath-yearimu.+
6 Na Daudi na Israeli wote wakapanda kwenda mpaka Baala,+ Kiriath-yearimu katika Yuda, ili kuleta kutoka huko sanduku la Mungu wa kweli, Yehova, anayekaa juu ya makerubi,+ ambalo jina lake limeitwa juu yake. 7 Hata hivyo, wakapandisha sanduku la Mungu wa kweli juu ya gari jipya la kukokotwa+ kutoka katika nyumba ya Abinadabu, na Uza na Ahio+ walikuwa wakiliongoza lile gari. 8 Na Daudi na Israeli wote walikuwa wakisherehekea+ mbele za Mungu wa kweli kwa nguvu kamili na kwa nyimbo+ na kwa vinubi+ na kwa vinanda+ na kwa matari+ na kwa matoazi na kwa tarumbeta.+ 9 Nao mwishowe wakaja mpaka uwanja wa kupuria wa Kidoni,+ na sasa Uza akanyoosha mkono wake ili kulishika lile Sanduku,+ kwa maana wale ng’ombe karibu waliangushe. 10 Ndipo hasira ya Yehova ikamwakia Uza, hivi kwamba akampiga kwa sababu alikuwa ameunyoosha mkono wake juu ya lile Sanduku,+ naye akafa hapo mbele za Mungu.+ 11 Na Daudi akakasirika+ kwa sababu Yehova alikuwa amemlipukia Uza, na mahali hapo pakaitwa Peres-uza mpaka leo hii.
12 Naye Daudi akamwogopa Mungu wa kweli siku hiyo,+ akisema: “Nitaliletaje sanduku la Mungu wa kweli kwangu?”+ 13 Na Daudi hakulileta Sanduku kwake katika Jiji la Daudi, bali alilichukua, akalipeleka kando kwenye nyumba ya Obed-edomu,+ Mgathi.+ 14 Nalo sanduku la Mungu wa kweli likaendelea kukaa pamoja na nyumba ya Obed-edomu, nyumbani kwake+ kwa miezi mitatu; na Yehova akazidi kuibariki+ nyumba ya Obed-edomu na vitu vyake vyote.