Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 35:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Mnapaswa kuchagua majiji yatakayowafaa ninyi ili yawe majiji ya makimbilio ili mtu anayemuua mwenzake bila kukusudia akimbilie humo.+

  • Hesabu 35:22-25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “‘Lakini ikiwa alimsukuma au kumtupia kitu chochote na kumuua bila kukusudia au bila chuki na bila nia mbaya,*+ 23 au ikiwa alimwangushia jiwe bila kumwona na mtu huyo akafa, lakini hakuwa adui yake au hakukusudia kumdhuru, 24 basi watu wanapaswa kuhukumu kati ya muuaji na mtu anayelipiza kisasi cha damu, kwa kufuata sheria hizo.+ 25 Kisha watu watamwokoa muuaji kutoka mikononi mwa mtu anayelipiza kisasi cha damu na kumrudisha katika jiji lake la makimbilio alimokuwa amekimbilia, naye atakaa humo mpaka kuhani mkuu aliyetiwa mafuta matakatifu+ atakapokufa.

  • Kumbukumbu la Torati 4:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Mtu yeyote anayemuua mwenzake bila kukusudia na hakuwa akimchukia,+ ni lazima akimbilie katika mojawapo ya majiji hayo ili aishi.+

  • Kumbukumbu la Torati 19:3-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Mnapaswa kugawanya mara tatu eneo la nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa mwimiliki, nanyi mtengeneze barabara ili muuaji yeyote aweze kukimbilia katika mojawapo ya majiji hayo.

      4 “Sasa hivi ndivyo itakavyokuwa kuhusu muuaji ambaye huenda akakimbilia humo ili kuokoa uhai wake: Akimuua jirani yake bila kukusudia naye hakuwa akimchukia;+ 5 kwa mfano, anapoenda na jirani yake msituni kukusanya kuni, kisha anainua mkono wake ili akate mti kwa shoka, lakini shoka lichomoke kwenye mpini na kumgonga jirani yake na kumuua, muuaji huyo anapaswa kukimbilia katika mojawapo ya majiji hayo.+

  • Yoshua 20:7-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Basi wakatenga majiji haya kuwa matakatifu: Kedeshi+ kule Galilaya katika eneo lenye milima la Naftali, Shekemu+ katika eneo lenye milima la Efraimu, na Kiriath-arba,+ yaani, Hebroni, katika eneo lenye milima la Yuda. 8 Na katika eneo la Yordani, upande wa mashariki wa Yeriko, wakachagua jiji la Beseri+ lililo nyikani kwenye uwanda wa juu katika eneo la kabila la Rubeni, Ramothi+ kule Gileadi katika eneo la kabila la Gadi, na Golani+ kule Bashani katika eneo la kabila la Manase.+

      9 Hayo ndiyo majiji yaliyochaguliwa kwa ajili ya Waisraeli wote na wageni walioishi kati yao, ili mtu yeyote atakayemuua mwenzake bila kukusudia akimbilie humo,+ ili asiuawe na mtu anayetaka kulipiza kisasi cha damu mpaka kesi yake isikilizwe mbele ya kusanyiko.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki