Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Pia, unapaswa kuadhimisha Sherehe ya Mavuno* ya matunda ya kwanza yaliyoiva* ya kazi zako, na ya vitu unavyopanda shambani;+ na Sherehe ya Kukusanya* mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mazao ya kazi zako.+

  • Hesabu 29:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “‘Na siku ya 15 ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu, nanyi mnapaswa kumfanyia Yehova sherehe kwa siku saba.+

  • Kumbukumbu la Torati 16:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Mnapaswa kufanya Sherehe ya Vibanda*+ kwa siku saba mnapokusanya nafaka kutoka katika uwanja wenu wa kupuria na kutoka katika shinikizo lenu la mafuta na divai.

  • Ezra 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kisha wakafanya Sherehe ya Vibanda* kulingana na ilivyoandikwa,+ na siku baada ya siku walitoa idadi iliyohitajika ya dhabihu za kuteketezwa.+

  • Nehemia 8:14-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kisha wakaona imeandikwa katika Sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa kwamba Waisraeli wanapaswa kukaa katika vibanda* wakati wa sherehe, mwezi wa saba,+ 15 na kwamba wanapaswa kutangaza+ katika majiji yao yote na kotekote Yerusalemu wakisema: “Nendeni katika eneo lenye milima mlete matawi ya mizeituni, ya misonobari, ya mihadasi na ya mitende, na matawi ya miti mingine yenye majani mengi ili mjenge vibanda, kama ilivyoandikwa.”

      16 Basi watu wakaenda kuleta matawi hayo ili kujijengea vibanda, kila mtu juu ya paa lake, na pia katika nyua zao, na katika nyua za nyumba ya Mungu wa kweli,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Maji,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Efraimu.+ 17 Basi watu wote wa kutaniko waliokuwa wamerudi kutoka utekwani wakajenga vibanda nao wakakaa katika vibanda hivyo, kwa maana Waisraeli hawakuwa wamefanya hivyo tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mpaka siku hiyo, basi wakashangilia sana.+ 18 Na siku baada ya siku kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kilikuwa kikisomwa,+ tangu siku ya kwanza hadi siku ya mwisho. Nao wakafanya sherehe hiyo kwa siku saba, na siku ya nane walifanya kusanyiko takatifu, kama ilivyoagizwa.+

  • Yohana 7:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Hata hivyo, Sherehe ya Vibanda ya Wayahudi,+ ilikuwa imekaribia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki