Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Pia, unapaswa kuadhimisha Sherehe ya Mavuno* ya matunda ya kwanza yaliyoiva* ya kazi zako, na ya vitu unavyopanda shambani;+ na Sherehe ya Kukusanya* mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mazao ya kazi zako.+

  • Mambo ya Walawi 23:34-36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Siku ya 15 ya mwezi huo wa saba mtamfanyia Yehova Sherehe ya Vibanda* kwa siku saba.+ 35 Mtakuwa na kusanyiko takatifu siku ya kwanza, nanyi hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu. 36 Kwa siku saba mtamtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko takatifu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Ni kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.

  • Kumbukumbu la Torati 16:13-15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Mnapaswa kufanya Sherehe ya Vibanda*+ kwa siku saba mnapokusanya nafaka kutoka katika uwanja wenu wa kupuria na kutoka katika shinikizo lenu la mafuta na divai. 14 Shangilieni wakati wa sherehe yenu,+ ninyi na wana wenu, mabinti wenu, watumwa wenu wa kiume, vijakazi wenu, Walawi, wakaaji wageni, mayatima, na wajane walio ndani ya majiji yenu. 15 Kwa siku saba mtamfanyia Yehova Mungu wenu sherehe+ mahali ambapo Yehova atachagua, kwa kuwa Yehova Mungu wenu atabariki mazao yenu yote na kila jambo mnalofanya,+ nanyi mtakuwa na shangwe kwelikweli.+

  • Nehemia 8:14-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kisha wakaona imeandikwa katika Sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa kwamba Waisraeli wanapaswa kukaa katika vibanda* wakati wa sherehe, mwezi wa saba,+ 15 na kwamba wanapaswa kutangaza+ katika majiji yao yote na kotekote Yerusalemu wakisema: “Nendeni katika eneo lenye milima mlete matawi ya mizeituni, ya misonobari, ya mihadasi na ya mitende, na matawi ya miti mingine yenye majani mengi ili mjenge vibanda, kama ilivyoandikwa.”

      16 Basi watu wakaenda kuleta matawi hayo ili kujijengea vibanda, kila mtu juu ya paa lake, na pia katika nyua zao, na katika nyua za nyumba ya Mungu wa kweli,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Maji,+ na katika uwanja wa jiji wa Lango la Efraimu.+ 17 Basi watu wote wa kutaniko waliokuwa wamerudi kutoka utekwani wakajenga vibanda nao wakakaa katika vibanda hivyo, kwa maana Waisraeli hawakuwa wamefanya hivyo tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mpaka siku hiyo, basi wakashangilia sana.+ 18 Na siku baada ya siku kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kilikuwa kikisomwa,+ tangu siku ya kwanza hadi siku ya mwisho. Nao wakafanya sherehe hiyo kwa siku saba, na siku ya nane walifanya kusanyiko takatifu, kama ilivyoagizwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki