Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 20:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Waambie Waisraeli, ‘Jichagulieni majiji ya makimbilio+ kama nilivyowaambia kupitia Musa, 3 ili mtu atakayemuua mwenzake* bila kukusudia au bila kujua akimbilie humo. Atakimbilia humo ili kumkwepa mtu anayetaka kulipiza kisasi cha damu.+

  • Yoshua 20:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Basi wakatenga majiji haya kuwa matakatifu: Kedeshi+ kule Galilaya katika eneo lenye milima la Naftali, Shekemu+ katika eneo lenye milima la Efraimu, na Kiriath-arba,+ yaani, Hebroni, katika eneo lenye milima la Yuda. 8 Na katika eneo la Yordani, upande wa mashariki wa Yeriko, wakachagua jiji la Beseri+ lililo nyikani kwenye uwanda wa juu katika eneo la kabila la Rubeni, Ramothi+ kule Gileadi katika eneo la kabila la Gadi, na Golani+ kule Bashani katika eneo la kabila la Manase.+

  • Yoshua 21:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nao wakawapa wana wa kuhani Haruni jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji,+ yaani, jiji la Hebroni,+ na malisho yake, pia Libna+ na malisho yake,

  • Yoshua 21:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Waliwapa jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji,+ yaani, jiji la Shekemu+ na malisho yake katika eneo lenye milima la Efraimu, Gezeri+ na malisho yake,

  • Yoshua 21:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Na Wagershoni+ wa koo za Walawi walipewa jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji katika eneo la nusu ya kabila la Manase, yaani, jiji la Golani+ kule Bashani pamoja na malisho yake, na Beeshtera na malisho yake—majiji mawili.

  • Yoshua 21:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Na katika eneo la kabila la Naftali: jiji la makimbilio+ kwa ajili ya muuaji, yaani, jiji la Kedeshi+ kule Galilaya na malisho yake, Hamoth-dori na malisho yake, na Kartani na malisho yake—majiji matatu.

  • Yoshua 21:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Na katika eneo la kabila la Rubeni: Beseri+ na malisho yake, Yahazi na malisho yake,+

  • Yoshua 21:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Na katika eneo la kabila la Gadi:+ jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji, yaani, jiji la Ramothi kule Gileadi+ na malisho yake, Mahanaimu+ na malisho yake,

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki