-
Hesabu 21:23, 24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapitie katika eneo lake. Badala yake, Sihoni akawakusanya watu wake wote kwenda kuwashambulia Waisraeli nyikani, akafika Yahazi na kuanza kupigana nao.+ 24 Lakini Waisraeli wakamshinda kwa upanga+ na kumiliki nchi yake+ kuanzia Arnoni+ mpaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu jiji la Yazeri+ linapakana na eneo la Waamoni.+
-
-
Yoshua 12:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Basi hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kumiliki nchi yao upande wa mashariki wa Yordani, kuanzia Bonde* la Arnoni+ hadi Mlima Hermoni+ na eneo lote la Araba kuelekea upande wa mashariki:+ 2 Mfalme Sihoni+ wa Waamori, aliyeishi Heshboni na kutawala kutoka Aroeri,+ kwenye ukingo wa Bonde* la Arnoni,+ na kutoka katikati ya bonde hilo, na nusu ya Gileadi hadi Bonde la Yaboki, kwenye mpaka wa Waamoni.
-