Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 17:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Basi akaenda na kufanya kama Eliya alivyosema; mwanamke huyo pamoja na Eliya na familia ya mwanamke huyo wakawa na chakula kwa siku nyingi.+ 16 Unga uliokuwa katika mtungi huo mkubwa haukwisha, na mafuta yaliyokuwa katika mtungi ule mdogo hayakwisha, kama Yehova alivyokuwa amesema kupitia Eliya.

  • 1 Wafalme 17:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Yehova akasikiliza ombi la Eliya,+ na uhai wa mtoto huyo ukamrudia, akawa hai tena.+

  • 1 Wafalme 17:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ndipo mwanamke huyo akamwambia Eliya: “Sasa ninajua kwamba kwa kweli wewe ni mtu wa Mungu+ na kwamba neno la Yehova kutoka kinywani mwako ni kweli.”

  • 1 Wafalme 18:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Karibu wakati wa kutoa toleo la nafaka la jioni,+ nabii Eliya akaja mbele na kusema: “Ee Yehova, Mungu wa Abrahamu,+ Isaka,+ na Israeli, acha leo ijulikane kwamba wewe ni Mungu katika Israeli na kwamba mimi ni mtumishi wako na kwamba nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.+

  • 1 Wafalme 18:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Ndipo moto wa Yehova ukashuka kutoka juu, ukaiteketeza hiyo dhabihu ya kuteketezwa,+ kuni, mawe, na mavumbi, nao ukayaramba maji yaliyokuwa mtaroni.+

  • 1 Wafalme 18:46
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 46 Lakini mkono wa Yehova ukaja juu ya Eliya, akajifunga vazi lake kiunoni, akakimbia na kumpita Ahabu na kutangulia kufika Yezreeli.

  • 2 Wafalme 2:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kisha Eliya akachukua vazi lake rasmi,+ akaliviringa na kuyapiga maji, nayo yakagawanyika kushoto na kulia, basi wote wawili wakavuka ng’ambo kupitia nchi kavu.+

  • 2 Wafalme 2:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Walipokuwa wakitembea, huku wakizungumza, kwa ghafla gari la moto na farasi wa moto+ wakawatenganisha, na Eliya akapanda kuelekea mbinguni* katika dhoruba ya upepo.+

  • Luka 1:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Pia, atamtangulia kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo ya akina baba kwa watoto+ na wale wasiotii kwenye hekima ya waadilifu, na kumwandalia Yehova* watu waliotayarishwa.”+

  • Yohana 1:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Huu ndio ushahidi aliotoa Yohana, Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu wakamuulize: “Wewe ni nani?”+

  • Yohana 1:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Nao wakamuuliza: “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Akajibu: “Mimi siye.” “Je, wewe ndiye yule Nabii?”+ Akajibu: “Hapana!”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki