-
1 Mambo ya Nyakati 29:21, 22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Nao wakaendelea kumtolea Yehova dhabihu na kumtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa+ siku iliyofuata, ng’ombe dume wachanga 1,000, kondoo dume 1,000, wanakondoo dume 1,000, na matoleo yake ya vinywaji;+ walitoa dhabihu nyingi sana kwa ajili ya Waisraeli wote.+ 22 Wakaendelea kula na kunywa mbele za Yehova siku hiyo kwa shangwe nyingi,+ nao wakamweka Sulemani mwana wa Daudi kuwa mfalme kwa mara ya pili na kumtia mafuta mbele za Yehova ili awe kiongozi,+ na pia Sadoki kuwa kuhani.+
-