2 Nami nikaona, na tazama! farasi mweupe,+ na yule aliyeketi juu yake alikuwa na upinde; naye akapewa taji,+ naye akaenda akishinda na kukamilisha ushindi wake.+
5 Na yule mwanamke akazaa mwana,+ wa kiume, atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.+ Na mtoto wake akanyakuliwa* mpaka kwa Mungu na kwenye kiti chake cha ufalme.
11 Nami nikaona mbingu imefunguliwa, na tazama! farasi mweupe.+ Na yule aliyeketi juu yake anaitwa Mwaminifu+ na wa Kweli,+ naye anahukumu na kupigana vita kwa uadilifu.+
15 Na kinywani mwake upanga mrefu mkali unachomoza,+ upanga ambao atatumia kuyapiga mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.+ Isitoshe, anakanyaga shinikizo la divai ya hasira ya ghadhabu ya Mungu Mweza-Yote.+