Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 39:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Kwa kweli, umefanya siku zangu ziwe chache tu;*+

      Na urefu wa maisha yangu kuwa si kitu mbele zako.+

      Kwa hakika kila mwanadamu, ingawa anaonekana yuko salama, si kitu ila pumzi tu.+ (Sela)

       6 Kwa hakika kila mwanadamu hutembea huku na huku kama kivuli.

      Hukimbia huku na huku* bila sababu.

      Hurundika mali, bila kujua ni nani atakayeifurahia.+

  • Mhubiri 2:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Lakini nilipofikiria kazi zote nilizofanya kwa mikono yangu mwenyewe na kazi yangu yote ngumu niliyofanya kwa jasho ili kuitimiza,+ niliona kwamba kila kitu kilikuwa ubatili, kukimbiza upepo;+ hakukuwa na kitu chochote chenye thamani ya kweli* chini ya jua.+

  • Mhubiri 2:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Nikachukia vitu vyote nilivyokuwa nimefanya kazi ngumu chini ya jua ili kuvipata,+ kwa sababu ni lazima nimwachie mtu atakayekuja baada yangu.+

  • Mhubiri 2:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Yeye humpa mtu anayempendeza hekima na ujuzi na shangwe,+ lakini humpa mtenda dhambi kazi ya kukusanya na kurundika tu, ili ampe yule anayempendeza Mungu wa kweli.+ Hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo.

  • Luka 12:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ndipo akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na mjilinde na kila aina ya pupa,*+ kwa sababu hata mtu anapokuwa na vitu vingi, uhai wake hautokani na vitu alivyo navyo.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki