Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 49:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Anaona kwamba hata watu wenye hekima hufa;

      Wapumbavu na wasiotumia akili huangamia pamoja,+

      Nao hulazimika kuwaachia wengine mali zao.+

  • Mhubiri 2:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Nikachukia vitu vyote nilivyokuwa nimefanya kazi ngumu chini ya jua ili kuvipata,+ kwa sababu ni lazima nimwachie mtu atakayekuja baada yangu.+ 19 Na ni nani anayejua ikiwa atakuwa mwenye hekima au mjinga?+ Lakini bado atamiliki vitu vyote nilivyotafuta kwa jitihada nyingi na hekima chini ya jua. Hilo pia ni ubatili.

  • Mhubiri 4:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kuna mtu aliye peke yake, asiye na rafiki yeyote; hana mwana wala ndugu, lakini kazi yake yote ngumu haina mwisho. Macho yake hayatosheki kamwe na utajiri.+ Lakini je, yeye hujiuliza, ‘Ninafanya kazi kwa bidii na kujinyima* vitu vyema kwa ajili ya nani’?+ Hili pia ni ubatili na ni kazi inayosikitisha.+

  • Luka 12:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 kisha nitajiambia:* “Una* vitu vingi vizuri ulivyokusanya kwa miaka mingi; starehe, ule, unywe, na ujifurahishe.”’ 20 Lakini Mungu akamwambia, ‘Wewe mpumbavu, usiku huu wanautaka uhai wako.* Basi, vitu ulivyohifadhi vitakuwa vya nani?’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki