-
Mhubiri 2:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Nikachukia vitu vyote nilivyokuwa nimefanya kazi ngumu chini ya jua ili kuvipata,+ kwa sababu ni lazima nimwachie mtu atakayekuja baada yangu.+ 19 Na ni nani anayejua ikiwa atakuwa mwenye hekima au mjinga?+ Lakini bado atamiliki vitu vyote nilivyotafuta kwa jitihada nyingi na hekima chini ya jua. Hilo pia ni ubatili.
-
-
Mhubiri 4:8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kuna mtu aliye peke yake, asiye na rafiki yeyote; hana mwana wala ndugu, lakini kazi yake yote ngumu haina mwisho. Macho yake hayatosheki kamwe na utajiri.+ Lakini je, yeye hujiuliza, ‘Ninafanya kazi kwa bidii na kujinyima* vitu vyema kwa ajili ya nani’?+ Hili pia ni ubatili na ni kazi inayosikitisha.+
-