Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 15:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Ndipo Samweli akasema: “Je, Yehova hupendezwa zaidi na dhabihu za kuteketezwa na dhabihu nyinginezo+ kuliko kuitii sauti ya Yehova? Tazama! Kutii ni bora kuliko dhabihu,+ na kusikiliza kuliko mafuta+ ya kondoo dume;

  • Methali 21:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Kutenda mambo manyoofu na ya haki

      Humpendeza Yehova zaidi kuliko dhabihu.+

  • Isaya 1:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Dhabihu zenu nyingi zina faida gani kwangu?”+ asema Yehova.

      “Nimetosheka na dhabihu zenu za kuteketezwa za kondoo dume+ na mafuta ya wanyama waliolishwa vizuri,+

      Nami sipendezwi na damu+ ya ng’ombe dume wachanga+ na wanakondoo na mbuzi.+

  • Mika 6:6-8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Nitakuja mbele za Yehova nikiwa na nini?

      Nitainama mbele za Mungu aliye juu nikiwa na nini?

      Je, nitakuja mbele zake nikiwa na dhabihu nzima za kuteketezwa,

      Nikiwa na ndama wenye umri wa mwaka mmoja?+

       7 Je, Yehova atapendezwa na maelfu ya kondoo dume,

      Na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+

      Je, nitamtoa mwanangu mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya uasi wangu,

      Uzao wa mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu?*+

       8 Ee mwanadamu, amekuambia yaliyo mema.

      Na Yehova anataka* nini kutoka kwako?

      Anataka tu utekeleze haki,*+ uthamini sana ushikamanifu,*+

      Na utembee kwa kiasi+ na Mungu wako!+

  • Mathayo 9:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Nendeni, basi, mkajifunze maana ya maneno haya: ‘Ninataka rehema, si dhabihu.’+ Kwa maana sikuja kuwaita waadilifu, bali watenda dhambi.”

  • Mathayo 12:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Hata hivyo, kama mngeelewa maana ya maneno haya, ‘Ninataka rehema+ si dhabihu,’+ hamngewalaumu watu wasio na hatia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki