Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 20:17-19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Alipokuwa akipanda kwenda Yerusalemu, Yesu akawaita faraghani wale wanafunzi 12 na kuwaambia wakiwa barabarani:+ 18 “Tazama! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi. Nao watamhukumia kifo+ 19 na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa ili wamdhihaki, wampige mijeledi, na kumuua kwenye mti;+ na siku ya tatu atafufuliwa.”+

  • Marko 8:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Pia, akaanza kuwafundisha kwamba Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na baada ya siku tatu atafufuliwa.+

  • Marko 9:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake na kuwaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu, nao watamuua,+ na ingawa atauawa, atafufuka baada ya siku tatu.”+

  • Luka 9:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 lakini akasema: “Lazima Mwana wa binadamu apatwe na mateso mengi, akataliwe na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na siku ya tatu atafufuliwa.”+

  • Luka 18:31-33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Ndipo akawaita kando wale 12 na kuwaambia: “Tazama! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yaliyoandikwa kupitia manabii kuhusu Mwana wa binadamu yatatimia.*+ 32 Kwa mfano, atatiwa mikononi mwa watu wa mataifa+ naye atadhihakiwa,+ atatendewa kwa dharau, na kutemewa mate.+ 33 Watampiga mijeledi, kisha watamuua,+ lakini siku ya tatu atafufuka.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki